OPPOSITION PARTY LEGAL OFFICER AND EAST SINGIDA MP, TUNDU LISSU HAS BEEN ARRESTED SOON AFTER ADRESSING HIS POLITICAL RALY IN HIS CONSTITUENT

0 comments



OPPOSITION PARTY LEGAL OFFICER AND EAST SINGIDA MP, TUNDU LISSU HAS BEEN ARRESTED SOON AFTER ADRESSING HIS POLITICAL RALY IN HIS CONSTITUENT. 
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amekamatwa na polisi muda mfupi baada ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa Ikungi, Singida.

Wakati Lissu akiwa mikononi mwa polisi, Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa jana alifanya mkutano wa hadhara na kusema hakuna wa kumpangia cha kuzungumza kwenye mikutano yake.

Kukamatwa kwa Lissu
Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema ndiye aliyetoa taarifa za kukamatwa kwake kwenye mtandao akisema: “Wakubwa sana salaam. Ninawaandikieni maneno haya nikiwa chini ya ulinzi wa polisi Singida.

" Nimemaliza kuhutubia mkutano wa hadhara mji mdogo wa Ikungi ambao ni makao makuu ya Jimbo langu la Singida Mashariki. Mara baada ya kushuka jukwaani nimefuatwa Regional Crimes Officer (RCO) wa Mkoa wa Singida aliyejitambulisha kwa jina la Babu Mollel na kunitaarifu kuwa ameelekezwa na Regional Police Commander (RPC) Singida nikamatwe apparently (dhahiri) kuna amri ya kunikamata iliyotoka Dar es Salaam.

 “Kwa hiyo niko nguvuni na ninasubiri maelekezo ya RPC juu ya wanakotakiwa kunipeleka. It’s likely (inawezekana) nitasafirishwa Dar usiku huu. In fact (hakika) ni usiku huu kwa taarifa za sasa hivi. Kwa vyovyote itakavyokuwa, there’s no turning back. There’s no shutting up (hakuna kurudi nyuma, hakuna kunyamaza).

"Nitapambana kutetea haki yetu ya kuwasema watawala popote nitakapokuwa, whether in freedom or in jail (niwe huru au jela)... Aluta continua!. "

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Thobias Sedoyeka  alithibitisha kukamatwa kwa Lissu lakini alikataa kutoa sababu za hatua hiyo.

Chadema jana jioni ilitoa taarifa kuhusiana na kukamatwa kwa Lissu ikisema: “Tunaweza kuthibitisha kwa vyombo vya habari kuwa Mwanasheria Mkuu wa Chama Mh. Tundu Lissu anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Singida kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.”

Taarifa hiyo iliyotolewa na Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene ilibainisha kuwa Polisi walimkamata jana jioni baada ya kumaliza mkutano wake wa hadhara alioufanya Ikungi jimboni kwake na kueleza kuwa viongozi wa chama hicho mkoani humo walikuwa polisi kuhakikisha anapata haki zake kama inavyostahili na kwamba ofisi ya katibu mkuu inafuatilia kwa ukaribu kujua sababu hasa ya kushikiliwa kwake na kutoa msaada wa haraka kadri itakavyohitajika.

Lissu amekuwa kwenye misukosuko na Jeshi la Polisi mara kadhaa na kwa siku za karibuni alikamatwa na kufikishwa mahakamani akituhumiwa kutoa maneno ya uchochezi kwenye gazeti la Mawio.

Sambamba na kesi hiyo, Lissu alikamatwa na polisi kwa madai ya kutoa maneno ya uchochezi baada ya kupata dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Msimamo wa Msigwa
Mkoani Iringa, Msigwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa kwanza wa kibunge tangu alipochaguliwa uliofanyika kwenye viwanja vya Mwembetogwa mjini hapa, alisema hakuna wa kumpangia hoja za kuzungumza kwenye mikutano yake.

Juzi, mbunge huyo alipewa barua na Jeshi la Polisi iliyoeleza kuwa imempa kibali cha kufanya mikutano hiyo, lakini ikimuwekea masharti mbalimbali likiwamo la kutozungumzia viongozi wengine na badala yake ajikite kwenye shughuli za maendeleo na kuchukua maoni ya wananchi anaowawakilisha.

Pia, alitakiwa kuhakikisha kuwa hakuna mtu kutoka nje ya Mkoa wa Iringa au eneo lolote lililo nje ya mamlaka atakayeruhusiwa kuzungumza.

Lakini jana akihutubia alisema: “Ninaona watu wote mna nyuso za hofu na mimi nimekuja kuwaondoa hofu …hakuna mtu mwenye mamlaka ya kunipangia cha kuzungumza, sipo hapa kwa matakwa ya polisi … mimi nipo kwa matakwa ya kisheria na ninazungumza kwa mamlaka mliyonipatia.

 “Pia Katiba inaeleza wazi mad raka na kinga ya Mbunge… mbunge anayo haki ya kuitisha na kufanya mkutano wa hadhara kwa mjibu wa sheria.”

Kuhusu Rais kuzuia mikutano ya vyama vya siasa, Msigwa alisema hakubaliani na hatua hiyo kwa madai kuwa kufanya hivyo ni ukiukaji wa Katiba ya nchi na Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 ambavyo nchi inayoongozwa chini ya utawala wa kidemokrasia inapaswa kuvifuata.

 “Ninamuunga mkono na ninampongeza Rais John Magufuli kwa kupambana na ufisadi, anapinga rushwa… lakini siungani naye kwa kitendo chake cha kukandamiza demokrasia nchini na niwaombe wananchi wa Iringa kuungana na mimi kumpinga mtu anayekandamiza demokrasia nchini,” alisema.

Kuhusu Serikali kuhamia Dodoma, mbunge huyo ambaye pia ni waziri kivuli wa Wizara ya Mambo ya Nje, alikosoa uamuzi huo akisema hajawahi kuona katika mipango yote iliyowasilishwa na Serikali bungeni inayoelekeza hilo.

“Serikali ilileta mpango wake wa miaka mitano, mwaka mmoja na Bajeti, hivi vyote vinaletwa bungeni na baada ya kujadiliwa na kupitishwa, vinatungiwa sheria ili viweze kutekelezwa hivyo vipaumbele vyake ni lazima vifiti kwenye mipango hiyo,” alisema Msigwa na kuongeza:

 “Lakini katika vyote vitatu vya mwaka huu, mpango wa miaka mitano, mwaka mmoja na hata katika bajeti ya mwaka huu sijaona mahali popote palipoandikwa kipaumbele cha Serikali ni kuhamia Dodoma.”

Msigwa alisema kuhamisha Serikali ni gharama kubwa na kuwataka wakazi wa Iringa na maeneo mengine kuhoji suala hilo kama ndicho kipaumbele cha maendeleo na mahitaji yao.

Alisema wamejipanga kufanya shughuli za maendeleo ikiwamo miradi ya barabara, kuboresha huduma za afya, usafi wa mazingira na miundombinu.

Mkutano huo ulihudhuriwa na madiwani wa halmashauri hiyo wakiongozwa na Mstahiki Meya, Alex Kimbe.


Read More »

THIS IS A NEW LOOK TO THI CELEBRITY FROM WCB IN TANZANIA. THE REASONS FOR THE LOOK ARE HERE

0 comments


 
THIS IS A NEW LOOK TO THI CELEBRITY FROM WCB IN TANZANIA. THE REASONS FOR THE LOOK ARE HERE
Huu ndio muonekano mpya wa mtindo wa nywele wa kijana Raymond wa wasafi,kijana anaye hit kwa sasa na ngoma yake ya natafuta kiki, Kwa Mimi ninavyoona kiukweli kwa muonekano huu wa mtindo wa nywele aliouweka naona hajapendeza kabisa ni bora angebaki na muonekano wa kawaida ulikuwa poa sana.
Je wewe unaonaje?


Read More »

TANZANIAN OPPOSITION PARTY LEADER, HON. FREEMAN MBOWE VISIT TO HON. JOB NDUGAI, THE SPEAKER, AFTER HIS RETURN FROM INDIA FOR MRDICAL CHECK UP.

0 comments



 

TANZANIAN OPPOSITION PARTY LEADER, HON. FREEMAN MBOWE VISIT TO HON. JOB NDUGAI, THE SPEAKER, AFTER HIS RETURN FROM INDIA FOR MRDICAL CHECK UP.
Kiongozi wa Kambi rasmi  ya Upinzani Bungeni Mhe Freeman Mbowe akisalimiana na Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai alipomtembelea nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam.Spika wa Bunge amerejea nchini hivi karibuni kutoka nchini India alipokwenda kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake.


Read More »

CORPORAL PUNISHMENT HAS LED THIS FORM FOUR STUDENT ADMITTED TO THE HOSPITAL IN MBEYA. TEACHERS BEAT HER AS ONE OF THEM WERE TOUCHING HER PRIVATE PARTS WHICH IS TYPICALLY SEXUAL HARASSMENT TO THIS STUDENT

0 comments


 
CORPORAL PUNISHMENT HAS LED THIS FORM FOUR STUDENT ADMITTED TO THE HOSPITAL IN MBEYA. TEACHERS BEAT HER AS ONE OF THEM WERE TOUCHING HER PRIVATE PARTS WHICH IS TYPICALLY SEXUAL HARASSMENT TO THIS STUDENT






Read More »

IS BARACK OBAMA BETRAYED? THE QUESTION COMES FOLLOWING HIS BROTHER, MALICK OBAMA TO DECLARE BACKING DONALD TRUMP IN UNITED STATES OF AMERICA PRESIDENTIAL RACE. A COUPLE OF REASONS ARE HERE.

0 comments


 
IS BARACK OBAMA BETRAYED? THE QUESTION COMES FOLLOWING HIS BROTHER, MALICK OBAMA TO DECLARE BACKING DONALD TRUMP IN UNITED STATES OF AMERICA PRESIDENTIAL RACE. A COUPLE OF REASONS ARE HERE.

Malik Obama is disappointed with his brother President Barack Obama so much that he has opted to support Donald Trump whom he will vote for come November 8th.
President Obama’s Kenyan half-brother Malik Obama has bought into Trump’s ideology “Make America Great Again”

Malik has caused a storm after he publicly declared his support for Republican presidential nominee, Donald Trump. In an interview with the Post from his home in Kogelo, Siaya County, Malik said that his brother President Obama had disappointed him and that he would vote for Trump. (Malik has a dual citizenship for Kenya and US.)

He cited six reasons why he will be voting Trump on November 8th.

1. Malik admires Donald Trump
Malik told the Post Donald Trump speaks from his heart adding that he was deeply disappointed by Democrats.
He particularly singled out his brother’s administration as the reason why he switched allegiance to Republican.

2. President Obama failed to prosecute Clinton over leaked mails
Democrat Presidential nominee Hillary Clinton was involved in email scandal back then when she was the Secretary of State.
Hillary emails were leaked when she used private e-mail servers instead of secured ones provided by the US government.
Even though FBI have recommended not prosecuting Hillary for the breach of security for using private e-mail servers, Malik Obama thinks his brother Barack should have pushed for the prosecution of Clinton.
“She should have known better as the custodian of classified information,” Malik told the Post.

3. President Obama and Clinton ‘killed’ Muammar Gaddafi
US was part of NATO-led coalition airstrikes in Libya that saw the death of Muammar Gaddafi and downfall of his administration in 2011.
Malik Obama is annoyed President Obama and Clinton killed the Libyan leader whom he called one of his best friends. (Fact: Gaddafi's convoy was hit by a French airstrike and then rebels killed him afterwards).
Malik dedicated his 2012 biography of his late father Barack Obama Sr. to Gaddafi for making the world a better place.

4. President Obama and Democrats are pro same-$ex marriage
A polygamous Malik Obama (has three known wives though there are claims he has 12) is opposed to same-$ex relationships which his brother President Obama and Democrats at large, have been advocating for.
Malik told the Post he felt like a Republican because they don’t stand for same-sex marriage.

5. President Obama wanted to shut Barack H. Obama Foundation
Malik Obama is director of Barack H. Obama Foundation, a controversial Virginia charity organization named after his father.
Malik started the foundation in 2008 with the aim of bringing development in K’ogelo village, Siaya County.
The charity came under fire when The Post revealed in 2011 that it was an off-the-books operation that hadn’t registered with the state of Virginia and didn’t have tax-exempt status from the Internal Revenue Service (IRS).
IRS later gave Barack H. Obama Foundation a clean bill of health sparking speculations President Barack Obama had intervened.
Even so, Malik claims President Obama hasn’t provided any assistance to Barack H. Obama Foundation and instead he (Barack) wanted to shut it down.
“My brother didn’t help me at all. He wanted me to shut it down when I set it up. He hasn’t supported me at all.” Malik was quoted by the Post.

6. President Obama didn’t support his bid for Siaya gubernatorial race in 2013
Malik Obama failed with honors when he vied for Siaya gubernatorial seat in 2013 after spending close to Kes 2 million in campaign. And he’s blaming President Barack Obama for failing to endorse him as Siaya governor.

Malik expected President Obama to be by his side in his bid to be Siaya governor having been the President’s best man in his wedding, besides being his brother.
But surely, politics in Siaya and the greater Luo nation are determined by who Raila Odinga says ‘Tosha’, There is no way President Obama would have helped Malik won the Siaya gubernatorial seat.
Malik plans to travel to US in November to vote for Trump. 


Read More »

NGUZA VICKING (BABU SEYA), A FAMOUS ARTIST IN TANZANIA WITH CONGO DRC ORIGIN, NOW IN CRITICAL SITUATION THAT HE IS ADMITED TO HOSPITAL FROM JAIL

0 comments


 

 NGUZA VICKING (BABU SEYA), A FAMOUS ARTIST IN TANZANIA WITH CONGO DRC ORIGIN, NOW IN CRITICAL SITUATION THAT HE IS ADMITED TO HOSPITAL FROM JAIL
Mwanamuziki nguli nchini anayetumikia kifungo cha maisha jela, Nguza Viking ‘Babu Seya’ anadaiwa yu taaban ambapo amekimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa matibabu.

Mwandishi wetu alimshuhudia Babu Seya akiwa Muhimbili chini ya ulinzi wa askari magereza watatu na wafungwa wengine watano katika Jengo la Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) huku akiwa amedhoofu.

Haikuweza kujulikana mara moja ugonjwa uliosababisha Babu Seya ahamishiwe Muhimbili kwa matibabu kwa sababu Jeshi la Magereza lina hospitali yake na mwandishi alipoomba kwa mmoja wa askari magereza ili aweze kumsalimia mwanamuziki huyo, hakupewa ruhusa.

Baadhi ya wananchi waliomshuhudia mwanamuziki huyo akiwa Muhimbili na kuingizwa katika chumba cha daktari namba 112 walisema, anavyoonekana ni dhahiri ni mgonjwa kwa sababu hakuwa mchangamfu kama ilivyo kawaida yake.

“Nguza (Babu Seya) mara nyingi huwa mchangamfu lakini leo amekuwa mnyonge, mwili umepungua na hata ngozi yake siyo ang’avu, bila shaka anaumwa sana,” alisema mwananchi mmoja hospitalini hapo.

Hata hivyo, mara baada ya matibabu, Babu Seya aliingizwa katika gari la magereza na kurudishwa Gereza la Ukonga kuendelea kutumikia kifungo chake.

Dodosadodosa ya mwandishi hospitalini hapo ili kujua kinachomsumbua Babu Seya, haikuambulia chochote kwani daktari mmoja alisema ni mwiko kwao kutaja ugonjwa wa mgonjwa bila ridhaa yake na ni kinyume cha maadili ya kidaktari.

“Umeniuliza anaumwa nini, kwanza mimi siye niliyemtibu lakini hata kama ningejua ugonjwa wa Babu Seya, siwezi kukuambia ni unethical (kinyume cha maadili). Lakini kweli ni mgonjwa na ndiyo maana ameletwa hapa kutibiwa,” alisema daktari huyo aliyekuwa nje ya jengo moja akizungumza na mwanamuziki huyo.

Juni 25, 2004, Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar, Eddy Lyamuya aliwatia hatiani Babu Seya na wanaye Papii Kocha kwa kupatikana na hatia ya kubaka na kulawiti watoto wa Shule ya Msingi Sinza-Mapambano, Dar na kuwafunga kifungo cha maisha jela huku rufaa ya kesi yao ikiwekwa kiporo kwenye Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu iliyopo jijini Arusha. 


Read More »

BONGO FLAVA MUSIC FANS IN SOCIAL NETWORKS UNREST ON PHOTOS SHOWING MR. TEMBA WEDDING ENVIRONMENT. IS IT TRUE THAT HE GOT MARRIED TO THIS LADY? MHUUU HAVE A LOOK ON EVERYTHING HERE....

0 comments


 

BONGO FLAVA MUSIC FANS IN SOCIAL NETWORKS UNREST ON PHOTOS SHOWING MR. TEMBA WEDDING ENVIRONMENT. IS IT TRUE THAT HE GOT MARRIED TO THIS LADY? MHUUU HAVE A LOOK ON EVERYTHING HERE....

 Mashabiki wa muziki katika mitandao ya kijamii wazipokea kiutofauti picha zinazomuonyesha msanii wa muziki kutoka TKM Wanaume Family, Temba akiwa amefunga ndoa.

Read More »